Natazama juu milimani; msaada wangu utatoka wapi? Msaada wangu watoka kwa Mwenyezi-Mungu, aliyeumba mbingu na dunia. Hatakuacha uanguke; mlinzi wako hasinzii. Kweli mlinzi wa Israeli hasinzii wala halali. Mwenyezi-Mungu ni mlinzi wako; yuko upande wako wa kulia kukukinga. Mchana jua halitakuumiza, wala mwezi wakati wa usiku. Mwenyezi-Mungu atakukinga na baya lolote; atayalinda salama maisha yako. Mwenyezi-Mungu atakulinda katika shughuli zako zote tangu sasa na hata milele.
![]() |
Shalom,Habari za Jumapili,Nimatumaini yangu wote mnaendelea vyema.. Huku kwetu hatujambo Mungu yu mwema sana.. Sina La zaidi nawatakia siku njema na Mungu awe nanyi... |
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.
No comments:
Post a Comment