Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday, 26 March 2020

Watoto na Malezi;Shule ya Nyumbani-Jikoni Leo;Ratiba Ya Chakula Na Rachel-siwa...







Ratiba ya chakula ya watoto Waswahili wakati huu Wa Shule Ya Nyumbani

 :8:30-Uji;wa-Mchele,wa-Dona,wa-urezi,wa-Muhogo n.k.

 :10:30-CHai/juisi; na-Mihogo,Viazi,Chapati,maandazi,                             Vitumbua n.k.

 :1:00-Ugali/wali,Ndizi/viazi,Makande n.k
         Mboga;Nyama/kuku/samaki,Maharage/kunde/mbaazi,
        Mboga za majani,bamia/mrenda n.k

 :4:00-Chai/juisi/maji;na kachori,visheti,katlesi,                                        Keki,Bagia/badia/bajia 🤷🏽‍♀️za dengu/kunde n.k

 :6:00-Wali,Tambi,chipsi(zege)n.k

       : Chakula cha mchana kama kimebaki kinaweza kuliwa ..
       :Matunda wakati wowote 🍎(Desert)upendavyo 🍮🍧
    :Jumamosi/jumapili,wajiachie tuu wanavyopenda -🍔🌭🌮
    :Kutupa chakula ni mwiko ..

   :Ratiba ya chakula kipindi hiki watoto wapo nyumbani 
   :Tujaribu kuwalisha kama waswahili 🤣kama itawezekana 🤔
     :
     :
  :Nimatumaini yangu wakirudi shule watakuwa wenye nguvu na        Afya Njema 💪🏽💃🏾...

  :Mzazi/Mlezi;unaweza kuongeza/kupunguza na kusahihisha                              nilipokosea.
 :Pia unaweza kuandaa ya kwako ili tupate kujifunza zaidi
 :Unaweza kunitumia kwa :E-mail;rasca@hotmail.co.uk

  :
  :
 : Angalizo;mimi si mtaalamu wa Chakula na Lishe..
                 Unaweza kufanya utafiti zaidi
                Kulingana na afya ya mtoto wako 🙏🏽


Imeandikwa na Rachel siwa 🙏🏽❤️
Asanteni.





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

No comments: