Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday, 12 May 2021

Jikoni Leo;Mboga za Kula na Ugali 9;Nyama

 



Jikoni Leo;Mboga za Kula na Ugali 9;Nyamna ;yakuokwa/choma/kukaanga/kuchemsha.. ;Nimeunga kutumia; Nyanya,situmii za kopo,na huwa simpenzi sana wa kuzisaga labda niwe na haraka sana,Namenya (kizamani🤣) ;kitunguu maji-cheupe, ;Kitunguu swaum sijui thoum 🙌🏽 Tangawizi,hivi nanunua nakusaga nyumbani 🤓 ;karoti ;hoho za rangi zote ;chumvi/maggi Ndimu/Limau ;Roiko/Simba mbili-siyo lazimaa ;pilipili mbuzi natupia karibu na mwisho ;Kupika/ Kuunga; Nyama nyekundu /unaweza tumia yoyote.. ;NyamaNimeosha ;Nikachemsha kwa chumvi/maggi,ndimu/limau ;Kitunguu swaumu/thoum ;Tangawizi ;Pilipili mtama/manga[blacpepper]...kwanza Baada ya Maji ya kuoshea kukauka nikaongeza maji kidogo (inategemea na ugumu wa nyama) Yalivyokauka nikaendelea kukaanga na Mafuta yake mpaka ikawa kavu.. nikakarangiza viungo kwa mafuta kidogo.. ;Nikaweka Nyama nikakaanga na viungo.. ;Nyanya nikaweka mwisho.. ;Kabla sijaokoa nikaweka tomato souse(ketchup)kidogooo ;Unaweza kuweka chill souse(ile ya Tanzania nikiwanayo huwa naweka hiyo) ;Unaweza kuweka tomato pure.. ;Kabla sijaokoa nikatupia pilipili.. ;Unaweza weka kabichi(Cabbege) Mkono mmoja isiive sana 😋.. Hayaaaah kazi kwenu mnaweza kuongezea ujuzi nilipokosea ;siyo mpenzi wa viungooo vingii kama unapenda wewe Rukhsa 🙏🏽 Jikoni leo;Mboga 10 za kula na Ugali 😋 : :Ugali una mboga zake jee wewe Unapenda mboga zipi kula na Ugali? :Mimi nitaweka hapa ninazo Zipenda na zinazo patikana hapa tulipo 😊 : 🙏🏽🇹🇿 Kitchen today #mboga10 Jikoni Leo 👩🏾‍🍳

No comments: